Thursday, July 28, 2011

Kamera Kutumika Goli za Utata

Halmashauri ya kimataifa ya chama cha mpira cha England itatoa uamuzi kama idhinishe mfumo huo ama la mnamo mwezi wa Machi 2012.

Ikiwa itathibitishwa basi kiongozi wa FIFA Sepp Blatter anasema ligi za soka zitaweza kuutumia mwanzoni mwa msimu wa 2012-13 endapo utakua hauna kasoro wala hautagharimu fedha nyingi.

Mkuu wa ligi ya Premier ya England, Richard Scudamore amesema kwamba watautumia mfumo huo mara tu utakapoidhinishwa.

Teknolojia ya goli kuidhinishwa.

Blatter aliongeza kusema kwamba teknolojia hiyo inaweza pia kutumika katika michuano ijayo ya kombe la dunia la mwaka 2014 nchini Brazil .

Kwa miaka mingi mkuu huyo wa Fifa amekua akipinga matumizi ya teknolojia katika eneo la goli lakini inaelekea alibadili mawazo yake baada ya mabishano makali kuzuka mnamo mwaka 2010.

 

No comments:

Post a Comment